VIDEO: “NILIKUWA NATAMANI KUPATA MUME AMBAYE ATANIJALI NA KUNIHESHIMU” – MADAM FLORA

Moja ya stori ambazo zinatengeneza headlines katika siku za hivi karibuni ni kuhusu muimbaji wa muziki wa Injili nchini Flora ambaye alikuwa mke wa Emmanuel Mbasha kubadili jina.

Muimbaji huyo sasa amewataka mashabiki wa muziki wake kumtambua kwa jina la Madam Flora ingawa amekiri kupata tabu sana kabla ya kufikia uamuzi huo wa kubadilisha jina ambalo lililikuwa limezoeleka kwa wapenzi wa muziki wa Injili ndani na nje ya Tanzania.

Ayo TV na millardayo.com leo April 28, 2017 imepiga stori na Madam Flora ambapo mbali na kuelezea ujio wake mpya akiwa na jina mpya, ameelezea pia mipango yake kuelekea ndoa yake atakayofunga mwishoni mwa wiki.

“Mwanzoni niliwaza kwamba marafiki zangu watalipokeaje, watu ambao wameshazoea watapokeaje. Lakini mwisho wa siku unajua pale ambapo unahisi amani ndani ya moyo wako kwamba nikifanya jambo fulani najisikia amani, basi fanya…” – Madam Flora.

Bonyeza play kutazama…

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0753 336 000

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.