BASHE AIJIA JUU SERIKALI YA KENYA

Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini, Hussein Bashe. 
Mbunge wa Nzega mjini, Hussein Mohamed Bashe amesikitishwa na Serikali ya Kenya kuweka zuio la kuingiza mitungi ya gesi inayotoka Tanzania kwa kusema ni vizuri nchi hiyo ikaheshimu mikataba ya 'East African Community (EAC)' . 

Bashe amesema hayo baada ya serikali ya Kenya kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Andrew Kamau kupiga marufuku uagizaji wa gesi ya kupikia kutoka Tanzania kupitia mipaka ya nchi hiyo. 

"Serikali ya Kenya imezuia gesi za matumizi ya nyumbani zinazotoka Tanzania kuingia Kenya ni vizuri Kenya ikaheshimu 'EAC treaty common'......Dar es salaam 'port and Cost' ya gesi inayotoka Tanzania ndiyo 'competetive edge' ya makampuni ya Tanzania dhidi ya yale ya Kenya uamuzi huu si sawa". Ameandika Bashe kupitia ukurasa wake wa twitter. 


Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0753 336 000

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.