WABUNGE WA UKAWA WAACHIWA HURU KWA KESI YA KUMSHIKA MATITI KATIBU TAWALA

WABUNGE UKAWA WAACHIWA HURU 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru wabunge wa Ukawa na makada wao waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando.

Hakimu Mkazi Mkuu,Huruma Shaidi amewaachia huru leo wabunge hao  baada ya kuwaona hawana kesi ya kujibu.

Hakimu Shaidi amesema katika ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashtaka  umeshindwa kuthibisha, hata  mlalamikaji Mmbando hakumbuki ni nani alimjeruhi.

Ushahidi wake ulielezea jinsi washtakiwa walivyojishughulisha na nyaraka siku ya tukio na siyo kumjeruhi.

Kuhusu kushikwa matiti, Hakimu Shaidi alisema;

 “Sijui alishikwa matiti na nani?”

 Kutokana na  ushahidi huo Hakimu  aliwaachia huru washtakiwa wote kwa kuwa hawana kesi ya kujibu.

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0753 336 000

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.