KUNA MBINU ZAKUTUMIA ILI CHAMA KIFUTWE - LIPUMBA



Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF anayetambulika na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa nchini Prof. Ibrahim Lipumba amesema ameandika barua maalumu kwa jukwaa la wahariri kuonesha kusikitishwa kwake na vurugu zilizotokea hivi karibuni katika mkutano wa CUF na kusababisha waandishi kufanyiwa fujo.
Prof Lipumba ameliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo ameyasema hayo katika mahojiano na mwandishi wa habari wa Azam Two na pamoja na mambo mengine amemtaka katibu mkuu wa CUF Maalim Seif wakae wazungumze ili wamalize tofauti zao na wakae wakijenge chama..
“Baada ya kulisikia hilo niliamua kuchukua jukumu la kuwaandikia Jukwaa la wahariri barua ambayo ipo mbioni kwenda kwenye ofisi zao kwamba mimi binafsi kama mwenyekiti wa CUF nalaani kitendo cha kupigwa kwa waandishi wa habari na nijambo ambalo hatulikubali kabisa, hatuwezi kujenga Demokrasia ikiwa waandishi wahabari hawafanyi kazi yao katika hali ya amani na utulivu”
“Vile vile kijana wetu amekatwa kisigino kwa panga na anavyo elewa yeye kijana aliyemkata anaitwa Mohamedi Mgonvi na taarifa hii imepelekwa kwenye vyombo vya dola kwaiyo vyombo vya dola inalishughulikia na tulitoa wito ambao ulitolewa na Mkurugenzi wetu wahabari na uwenezi”
“Mimi toka awali nimeeleza kwamba nataka tumalize tofauti za kisiasa kwa mazungumzo tupate suluhu tuheshimu katika ya chama chetu na nimekuwa nikimuita Maalim Seif aje ofisi bugurudi aweze kuzungumza afanye kazi zake kama katibu mkuu na mimi nimemfahamu Maalim Seif mwaka 1973 tukiwa wanafunzi wa chuo kikuu Dar es Salaam kwahiyo hatuna sababu ya sisi kuwa na mgogoro huu na kuuruhusu kuendelea”
“Hivi sasa kupitia taarifa zetu zakiuchunguzi zinaonesha kwamba kuna mbinu yakutaka chama hiki kiweze kufutwa kwaiyo kuna matukio ya napangwa njee ya chama ili paweze kutokea vurugu nazikishatokea waseme chama hiki hakifai kuendelea kuwa chama cha siasa na utakuta kuna vyama vingine vya siasa vinashabikia na kutoa wito ilichama hichi kiweze kufutwa” Prof. Lipumba
VIDEO: Waandishi walioshambuliwa kwenye vurugu za CUF wasimulia

VIDEO: Msimamo wa Jukwaa la Wahariri kwa CUF baada ya kushambuliwa wanahabari. Bonyeza play kutazama…

TUPIA COMMENTS
)
:)

Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0753 336 000

Masengwa blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari zote kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa

No comments:

Powered by Blogger.